We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Thursday, July 11, 2019

Dk Bashiru: Msiihusishe Serikali na matukio ya watu kutekwa, kupotea



Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) nchini Tanzania, Dk Bashiru Ally amesema si sahihi kuihusisha Serikali ya Tanzania na matukio ya utekaji wa watu.

Ametoa kauli hiyo leo Alhamisi Julai 11, 2019 katika kata ya Naisinyai wilayani Simanjiro katika siku yake ya kwanza ya ziara yake mkoani Manyara.
Amebainisha kuwa baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa wanatoa taarifa potofu kuhusu watu wanaotekwa na kupotea na kuhusisha matukio hayo na Serikali.
"Ulinzi na usalama ni wajibu wa Serikali, baadhi ya watu kuihusisha (Serikali) na watu wasiojulikana wanaoteka watu hapo watakuwa wanaoichonganisha na watu wake," amesema Bashiru huku akibainisha kuwa mwenye jukumu la kutoa taarifa katika Mkoa ni Mkuu wa Mkoa na kamanda wa polisi wa Mkoa.
“Hao wawili ndio wanapaswa kutoa taarifa ya hali ya ulinzi na usalama ya Mkoa na si viongozi wengine wanaochafua hali ya hewa kwenye mitandao ya kijamii," amesema Bashiru.


Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti akisoma taarifa ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya Mkoa huo amesema Serikali imepiga hatua kwenye miradi mbalimbali ikiwemo ya elimu, afya, miundombinu ya barabara, umeme na maji.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list