Jana uongozi wa Simba ulitoa taarifa ya kujiuzulu kwa aliyekuwa Mwenyekiti wa timu hiyo Swedi Mkwabi
Simba inasubiriwa kuweka hadharani utaratibu wa kumpata Mwenyekiti mwingine atakayechukua nafasi ya Mkwabi
Inaelezwa kuna uwezekano mkubwa aliyekuwa Mwenyekiti kabla ya Mkwabi, Salum Abdallah 'Try Again' akarejea katika nafasi hiyo baada ya Wajumbe wengi wa Bodi ya Wakurugenzi kuonyesha imani kubwa kwake
Hata hivyo Try Again ni mmoja wa Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi akipata nafasi hiyo kupitia upande wa Mwekezaji Mohammed Dewji 'Mo'
Lakini kazi yake nzuri aliyofanya wakati akiwa Mwenyekiti wa Simba, inampa nafasi kubwa ya kurejea tena kwenye majukumu hayo kama atachukua fomu mchakato utakapoanza

No comments:
Post a Comment