We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Thursday, August 29, 2019

Paul Makonda azindua 'Pekenyua Tukufukunyue'

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda kwa kushirikiana na Idara ya Uhamiaji nchini, wamezindua mpango wa kutokomeza wahamiaji haramu mkoani humo alioupa jina la ''Pekenyua Tukufukunyue''.

Mpango mkakati huo umezinduliwa leo Agosti 29, na kuwataka viongozi wote wa mitaa kuhakikisha wanaweka mifumo rasmi itakayomtambulisha mwananchi wa eneo lake, jambo litakalosaidia kuondoa uhalifu pamoja na wananchi kutoa taarifa pindi wanapobaini uwepo wa mtu wanayemtilia mashaka.
''Wahamihaji haramu nchini ni jambo la hatari kiusalama kwakuwa baadhi yao wanafanya uhalifu wa Wizi, Ubakaji, Uporaji, wanatumia rasilimali za nchi, wanatumia fursa ambazo zilipaswa kuwanufaisha wazawa ikiwemo Afya, Elimu na Ajira, kusababisha msogamano wa watu magerezani pamoja na kuwa Chanzo cha Migogoro'' amesema RC Makonda.
Kutokana na hilo Makonda ameviagiza vyombo vyote vya ulinzi na usalama, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri, Viongozi wa Kata na Mitaa kuhakikisha Mpango huo unafanikiwa kwa 100%.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list