We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Saturday, August 3, 2019

Dk Bashiru: Wanawake wanaipenda zaidi CCM


Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) nchini Tanzania, Dk Bashiru Ally amesema chama hicho kinapambwa na kupendwa zaidi na wanawake.

Ametoa kauli hiyo leo Jumamosi Agosti 3, 2019 wakati akizungumza na seneti ya wanafunzi wa vyuo vikuu Mkoa wa Mwanza na kubainisha kuwa chama kinachopendwa na wanawake ni ngumu kukishinda.
“Wanawake wanaongoza kwa kukipamba CCM, chama kikipendwa na wanawake na vijana ndio uhai wake na huwezi kukishinda,” amesema Dk Bashiru
Amesema licha ya uhai wa chama kutegemea wanachama wengi na wapya lakini hawataki wanaoendekeza maslahi yao binafsi bali wanaoweza kujitolea na kukijenga.
Akizungumzia kuhusu chaguzi zijazo ukiwemo wa Serikali za mitaa, Dk Bashiru amesema atakayetumia ukabila, fedha na maslahi binafsi hatavumiliwa.
Amewataka viongozi wa siasa kufuata demokrasia za uchaguzi akidai maadui wa ndani na nje ya nchi wapo na wanaweza kuvuruga amani ya Taifa.
“Atakayetumia uchaguzi kutugawa huyo ni adui wetu, wakati wa uchaguzi ni wakati wa kutafuta viongozi bora na wala sio wa kutafuta machafuko. Wapo ambao wameanza chokochoko, mimi nimewaangalia tu na nimewakalia kimya, wakija hapa Mwanza waone kama adui yenu.”
“Ubepari na ubeberu haujaisha nchini tusipojipanga mikakati hatutaweza kushinda kwenye uchaguzi huo,” amesema Dk Bashiru.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list