We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Tuesday, July 9, 2019

Yanga yazungumzia Gadiel Michael kutimkia Simba

Uongozi wa Yanga umezungumza kwa mara ya kwanza kufuatia kuondoka kwa mlinzi wake kisiki, Gadiel Michael ambaye ametimkia kwa mahasimu wao Simba.

Gadiel Michael ametambulishwa hii leo na klabu ya Simba kuwa mchezaji wake rasmi kwa mkataba wa miaka miwili.
Uongozi wa Yanga kupitia kwa Meneja wake, Hafidh Saleh umesema kuwa wao kama klabu wameshamsahau Gadiel kwakuwa wameshasajili wachezaji bora kuelekea msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania bara.
"Gadiel Michael alikuwa mchezaji wetu, amemaliza kandarasi yake na hakupenda kuongeza mkataba ameamua kuondoka, kwahiyo kuna maisha mengine. Sisi tumeshamsahau ni kama historia kwetu", amesema Hafidh Saleh.
Pia Hafidh amezungumzia maandalizi kamili ya kikosi cha Yanga kuelekea ufunguzi wa ligi mwishoni mwa mwezi ujao, ambapo amesema kikosi kamili pamoja na kocha Zahera watawasili wiki ijayo.
Tazama video hapa chini akizungumza zaidi.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list