We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Thursday, July 4, 2019

Waziri Mhagama: Watanzania changamkieni fursa bomba la mafuta


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye ulemavu wa Tanzania, Jenister Mhagama amewataka Watanzania wanaoishi mikoa inayopita bomba la mafuta kutoka nchini Uganda, kuchangamkia fursa za kiuchumi zinazotokana na mradi huo.

Akifungua kongamano la Baraza la Taifa la Uwezeshaji wananchi kiuchumi linalofanyika mjini Shinyanga jana Julai 3, 2019, Mhagama ametaja fursa zinazoambatana na mradi huo unaopita kwenye mikoa minane kuwa ni pamoja na ajira, biashara na huduma mbalimbali za chakula, malazi na makazi kwa watumishi.
“Watanzania watakaopata fursa ya ajira katika mradi huu, watumia nafasi hiyo kujifunza na kupata ujuzi na teknolojia mpya kutoka kwa wageni watakaoajiriwa katika mradi huu,” amesema Mhagama.
Katibu mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji wananchi kiuchumi, Beng’I Issa ametaja sekta ya ujenzi, afya, kilimo (chakula), mawasiliano na huduma za kijamii kuwa miongoni mwa maeneo muhimu yatakayonufaika.
“Asilimia 60 ya kazi ya ujenzi wa bomba hilo la mafuta itafanyika upande wa Tanzania huku asilimia 40 inayosalia, ndiyo itahusu upande wa Uganda. Tuchangamkie fursa hiyo,” amesema Issa.
Kwa upande wa Tanzania, mradi huo unapita kwenye mikoa minane, wilaya 24 na vijiji 134 ambako nafasi za ajira ya muda zaidi ya 10,000 na nyingine 1,000 za kudumu zinatarajiwa kupatikana maeneo hayo huku moja kati ya vituo vinne vya ujenzi kinatarajiwa kujengwa wilaya ya Nzega mkoani Tabora.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack amewataka wakazi mkoani humo kujipanga kutumia kila aina ya fursa itakayojitokeza huku Mwenyekiti wa Bodi ya Haki Rasilimali, Dolnad Kasongi akiahidi kuwa bodi hiyo itatoa elimu kwa wananchi katika maeneo bomba hilo linakopita ili waweza kutumia fursa za kiuchumi zitakazojitokeza.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list