We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Wednesday, July 24, 2019

Rais Magufuli kuzindua mradi wa umeme Mto Rufiji Julai 26, 2019

Waziri wa Nishati nchini Tanzania, Dk Medard Kalemani amesema Rais wa Tanzania, John Magufuli keshokutwa Ijumaa Julai 26, 2019 ataweka jiwe la msingi katika Mradi wa  kufua umeme wa megawati 2115 wa Rufiji ‘Stigler's Gorge’ uliopo mikoani ya Pwani na Morogoro.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatano Julai 24, 2019 Morogoro, Waziri Kalemani amesema tukio hilo kubwa la kihistoria kukamilika kwake kutawezesha Taifa Kuwa na umeme wa kutosha, wa uhakika, unaotabirika na hatimaye kuwa wa gharama nafuu kwa watumiaji.

Amesema wizara inawahakikishia Watanzania kuwa utekelezaji wa mradi huo ni wa kasi, weledi na nidhamu na hiyo ni katika kuunga mkono juhudi za Serikali inayongozwa na Rais Magufuli.

Mradi huo mkubwa wa umeme utakapokamilika unatarajia kutumia kiasi cha Sh6.5 trilioni ambazo ni fedha za Serikali ya Tanzania.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list