We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Wednesday, July 24, 2019

NEMC yawanyooshea kidole wenye baa, kundi za muziki


Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) nchini Tanzania, limewataka wamiliki wa baa na kumbi za starehe kupiga muziki kwa sauti ndogo ili  kuondoa bugudha kwa wakazi wanaoishi karibu na maeneo yao ya biashara.

Kauli hiyo imetolewa baada ya baraza hilo kupokea malalamiko ya wananchi kuwa baa na kumbi hizo za starehe zinapiga muziki kwa sauti kubwa.
Hayo yameelezwa leo Jumatano Julai 24, 2019 katika mkutano wa baraza hilo  uliolenga kuwaelimisha wamiliki wa baa na kumbi za starehe na sherehe namna ya kuepukana nazo.
Akizungumza katika mkutano huo, Mkurugenzi wa NEMC, Dk Samuel Gwamaka amesema katika kipindi cha mwezi mmoja uliopita alipokea zaidi ya malalamiko 100 ya kelele kutoka kwa wananchi.
“Sasa kelele hizo zina athari mbalimbali kwa jamii iliwemo kusababisha magonjwa sababu kitu chochote unachokifanya wewe siyo wote wanakifurahia,” amesema
Amesema kama baraza pia linahusika katika utoaji wa vibali vya matamasha mbalimbali kwa kuzingatia muda maalumu wa kufanyika kwa tamasha hilo, kiwango cha kelele kitakachozalishwa.
Naye  Meneja wa Tips bar iliyopo Mikocheni, Dar es Salaam, Ismail Kagambo amesema elimu hiyo ilipaswa kutolewa miaka mingi nyuma ili wajue namna wanayoweza kuepuka hali hiyo.
“Huwa tunapokea malalamiko mengi kutoka kwa majirani zetu, tumekuwa tukikaa nao na kuwaeleza hali halisi lakini pia Nemc inapaswa kupita na kwa jamii inayotunguka kuwapitia elimu hii,” amesema Kagambo.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list