We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Friday, July 12, 2019

Polisi Pwani yaua majambazi wanne

Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani, limefanikiwa kuua majambazi wanne katika tukio la majibizano ya risasi, baina ya polisi na majambazi hayo huko eneo la Kwala, Wilaya ya Kipolisi Mlandizi.

Taarifa hiyo imetolewa na Kamanda wa polisi mkoani humo, Wankyo Nyigesa, ambapo amesema, tukio hilo limetokea Julai 11,2019, majira ya saa 8 mchana baada ya kupata taarifa ya uwepo wa watu, waliopanga kwenda kuvamia na kupora fedha za malipo, kwa wafanyakazi wanaojenga Bandari Kavu ya Kwala.
"Jeshi la Polisi Mkoani hapa tuliweka mtego, na majambazi hao kujikuta wakinasa, na kuanzisha majibizano ya risasi na kupelekea majambazi wanne, kati ya sita wanaodhaniwa kuwepo kupoteza maisha" amesema RPC Wankyo.
Katika tukio hilo, majambazi hao wamekutwa wakiwa na bunduki mbili aina ya Pump action, Radio call moja, hirizi, dawa za kupulizia watu, kamba za kufungia watu na, Plasta za kuziba watu midomoni.
Vitu vingine ni pamoja na leseni za udereva, vitambulisho mbalimbali vya uraia, kadi ya bima ya afya, koti, kaniki, kanzu, suruali na kaptula .
Miili ya majambazi hao, imehifadhiwa katika hospitali ya rufaa ya Mkoa ya Tumbi.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list