We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Monday, July 29, 2019

Mtatiro aanza kivingine Tunduru

Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Julius Mtatiro, amewakaribisha wawekezaji nchi nzima kujitokeza kuwekeza wilayani Tunduru, akisema kuwa Wilaya yake imetenga kiasi kikubwa cha ardhi kwa uwekezaji.

Mtatiro ametoa kauli hiyo ikiwa ni siku chache tangu aapishwe kuwa Mkuu wa Wilaya hiyo, ni kuanza utekelezaji wa agizo la Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, aliloltoa hivi karibuni wakati akizindua fursa za uwekezaji mkoani Ruvuma.
"Tunduru tuna maeneo ya uwekezaji tena uwekezaji wa kutosha, tumetenga maeneo ya kutosha kwa ajili ya kuwekeza, sasa maeneo yote yameshatengwa na mwekezaji akija hapa kwetu tunampa hati ya eneo anaenda kuanza kazi.", amesema Julius Mtatiro.
Hivi karibuni akiwa mkoani Ruvuma, Waziri Mkuu Majaliwa aliwataka Wakuu wa Mikoa kutenga wiki maalum kwa ajili ya kuitumia kuitangaza Mikoa yao, juu ya fursa za uwekezaji zilizopo kwenye mikoa yao.
Julai 14, Rais wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli alitangaza kumteua Julius Mtatiro kuwa Mkuu wa Wilaya ya Tunduru akichukua nafasi ya aliyekuwa Mkuu wa Wilaya hiyo Juma Homera ambaye aliteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list