We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Tuesday, July 2, 2019

Membe Ashangaa Tundu Lissu Kuvuliwa Ubunge.... Azungumzia Matukio ya Utekaji Nchini

Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Benard Membe amewataka viongozi wa dini, serikali na wastaafu kukemea suala la utekaji kwani haiwezekani watu kuishi nchini kwa wasiwasi.

Amezungumza hayo leo  na waandishi wa habari katika viunga vya Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam  wakati alipokuja kusikiliza kesi ya madai aliyofungua dhidi ya mmiliki wa gazeti la Tanzanite, Cyprian Musiba na wachapishaji wa gazeti hilo.
 
“Huu ni utamaduni mpya ambao haukubaliki na ningependa kuchukua nafasi hii kusema kwamba suala la utekaji na watu kupotea linaweza kuiondolea nchi yetu heshima duniani tangu tupate uhuru, hivyo ningependa kuwaomba viongozi wote walikemee,”

“Viongozi wa serikali wasione aibu hata wa Dini wasiogope na wastaafu wote lazima tukemee utamaduni huu mpya, hatuwezi kuendelea kuishi katika nchi yenye watu wenye wasiwasi na uoga ambao hawajui kesho wataamka vipi na hii ajenda iishe maana isipo isha itaenda kwenye uchaguzi mwakani,” Membe

Aidha, akizungumzia kuhusu Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu kupoteza ubunge, Membe amesema kama Mtanzania ameshangaa sana.

“Mimi kama Mtanzania  nilishangazwa sana na uamuzi wa Spika, Job Ndugai lakini tusubiri Lissu arudi.

“Nina uhakika atakwenda mahakamani kudai haki yake na kama ipo haki ataipata mahakamani,” amesema Membe



Membe

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list