We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Tuesday, July 2, 2019

Dengue yaahirisha kesi ya viongozi wa CHADEMA

Kesi namba 112 ya mwaka 2018 inayowakabili Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe pamoja na viongozi wengine saba wa chama hicho imeahirishwa leo Juni 2 2019 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Kesi hiyo inayowajumuisha Ester Matiko, John Mnyika na Grace Kiwelu inayohusu kufanya mkusanyiko usio halali, imeahirishwa baada ya shahidi wa 6, Koplo Charles kuzidiwa akiwa kizimbani.
Akiongozwa na wakili wa serikali Kadushi kutoa ushahidi wake, Dengue yatajwa kuwa sababu ya kesi hiyo Kuahirishwa.
Shahidi Koplo Charles alizidiwa akiwa Kizimbai ambapo alidai hajisikii vizuri baada ya kulazwa wiki iliyopita akisumbuliwa na Ugonjwa wa Dengue
Baadhi ya mashtaka waliyosomewa ni kula njama na kufanya mkusanyiko usio halali, wenye ghasia na kukiuka tamko la kutawanyika na kusababisha watu waogope. Tukio hilo lilifanyika Februari 16, 2018 katika barabara ya Kawawa Kinondoni Mkwajuni Jijini Dar es salaam.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list