We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Saturday, July 27, 2019

Mbatia ampongeza Rais Magufuli, “Amefanya makubwa yenye uthubutu hata wengine hawawezi”

Mwenyekiti wa Chama cha NCCR- Mageuzi, James Mbatia amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli kwa jitihada zake za kudhibiti vitendo vya rushwa, uhalifu, utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa miundombinu ya reli ya kisasa, upatikanaji wa elimu bure.
Mbatia ambaye pia ni mbunge wa Vunjo amesema hayo leo Julai 27, 2019 jijini Dar es Salaam katika mkutano mkuu wa chama hicho kwa ajili ya kuchagua viongozi wapya wa chama hicho.
Amepongeza Serikali na hatua nyingine kadhaa ikiwemo uthubutu wa kutekeleza mambo mbalimbali katika kipindi cha miaka minne tangu Rais Magufuli alipoapishwa Novemba 5, 2015.
“Rais Magufuli ni mwenye uthubutu na amefanya makubwa yenye uthubutu hata wengine hawawezi kufanya.”
Aidha, Mbatia amemuomba Rais Magufuli aridhie uwepo wa meza ya maridhiano ya vyama vya siasa ili kujenga nyumba moja.
“Basi athubutu kutukalisha tuzungumze ili tuwe na mifumo imara na taasisi imara na endelevu kwa maslahi mapana ya mama Tanzania, mimi niko tayari tuyazungumze,” amesema Mbatia.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list