We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Saturday, July 27, 2019

Mo Dewji avunja ukimya, aweka wazi kuhusu Simba

Mfanyabiashara Mohammed Dewji amesema haondoki Simba na tayari wameshaongea na serikali na kwamba maendeleo ya mpango wa uwekezaji kwenye klabu hiyo unaendelea vizuri.

Mo Dewji ambaye kwasasa anatambulika kama Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Simba amesema amesikitishwa na baadhi ya mambo yanayoendelea mtandaoni ikiwemo kusema Waziri wa Michezo Harrison Mwakyembe ameanzisha utaratibu mpya.
''Nimesikitishwa na mijadala mitandaoni ya kumshutumu Waziri Mwakyembe kwamba ameanzisha utaratibu mpya wa mwekezaji kuwa na 49% na wanachama 51% ya hisa. Ndugu zangu, si kweli. Utaratibu huu upo tangu 2017 kisheria na sisi Simba tulikubali'', ameandika.
Aidha Mo Dewji amesisitiza kuwa, ''Waziri Mwakyembe alituruhusu SIMBA tuendelee na mwekezaji mmoja. Ndugu WanaSimba Mimi nipo na niko na nyinyi, siendi popote. Na sasa tumeishazungumza na Serekali na mazungumzo ni mazuri.
Mbali na hilo mfanyabiashara huyo na mpenzi wa mpira wa miguu hapa nchini amewasihi mashabiki wa Simba kujitokeza kushangilia taifa Stars kwenye mechi ya kesho kuwania kufuzu CHAN 2020 dhidi ya Kenya.
''Nawasihi WanaSimba wote twendeni tukaishangilie Timu ya Taifa na tukutane Simba Day tarehe 6. Tulianza vizuri na Serikali na tutamaliza vizuri na Serikali''.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list