We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Thursday, July 11, 2019

Lugola Awataka Watanzania Wawe na utamaduni wa kushirikiana na Serikali Katika Miradi ya Maendeleo

Na Felix Mwagara, Mwibara (MOHA)
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, amewataka wananchi nchini wawe na utamaduni wa kushirikiana na Serikali kujenga shule, zahanati, vituo vya polisi katika maeneo wanayoishi kuliko kuwa na akili potofu miradi hiyo inajengwa na Serikali pekee.

Lugola ameyasema hayo wakati akikagua miradi mbalimbali ya maendeleo jimboni kwake Mwibara, Wilaya ya Bunda, Mkoani Mara, leo, ambapo pia alishirikiana na wananchi wa Kijiji cha Namalebe kushiriki ujenzi wa shule mpya ya msingi ya Ibwagulilo iliyopo katika Kata ya Chitengule jimboni humo ambayo Serikali imetenga shilingi milioni 96 kwa ajili ya kuikamilisha shule hiyo.

“Mradi huu unaendelea vizuri, ambapo Serikali imetupa milioni 96.9 kuukamilisha mradi huu, nami nipo hapa na nimeshirikiana na wananchi wangu kujitolea kujenga shule hii ambayo itawasaidia wananchi wa Kata hii ili Watoto wao waweze kupata elimu,” alisema Lugola.

Waziri Lugola pia aliwahamasisha wananchi hao kushiriki matukio ya maendeleo, pia alitoa mabati, saruji, nondo kwa ajili ya ujenzi wa zanahati, na kuongeza madarasa katika shule mbalimbali zilizopo katika jimbo lake.

Naye Fundi Mkuu wa Shule ya Msingi, Marco Malima, alimshukuru Waziri huyo kwa kufika katika eneo la ujenzi huo na imewapa nguvu zaidi kufanikisha ujenzi huo kwa wakati.

“Fedha na vifaa kukamilisha ujenzi huu zipo, ujenzi huu ulianza mwezi mei mwaka huu na unatarajiwa kukamilika mwezi wa saba mwaka huu, ambapo tunajenga madarasa, nyumba za walimu pamoja na vyoo,” alisema Malima.

Waziri Lugola anaendelea na ziara ya kutembelea miradi ya maendeleo jimboni humo pamoja na kuzungumza na wananchi na kutatua kero zao zinazowakabili.

Lugola amewataka wananchi wa jimbo lake, waendelee kumuamini na kushirikiana naye wakati wanahakikisha jimbo hilo linakua jipya zaidi kimaendeleo.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list