We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Thursday, July 4, 2019

'Kuna watu walianza kuomba Taifa Stars ifungwe'' Makonda

Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda, amewataka watanzania kuacha makundi na kuwa pamoja kwenye nyakati zote hususani mambo ya kitaifa, kama ushindi wa Taifa Stars ambao sio wa Makonda peke yake.

Makonda ameyasema hayo kwenye mapokezi ya Taifa Stars kwenye uwanja wa ndege wa JK Nyerere, ambapo ameeleza kuwa timu hiyo inahitaji pongezi na kujipanga kwaajili ya michuano mingine kama CHAN.
''Ilifika wakati watu wakawa wanaona kama hii ni timu ya Makonda na kuomba pengine ifungwe, lakini ikishinda inakuwa ni timu ya taifa, naomba tuache hiyo tabia tuwe tunaitumia taifa Stars kuwa wamoja na kuwajenga wachezaji wetu'', amesema.
Aidha Mkuu huyo wa Mkoa ameeleza kuwa anazo taarifa amezibaini kule nchini Misri kuwa kuna taasisi ilichangisha fedha kwaajili ya Taifa Stars lakini haikuziwakilisha na badala yake wao wakazitumia kwenda kufanya starehe Misri.
''Wanajijua niwaombe tu kama ambavyo akaunti imetangazwa na Waziri wa Michezo wazifikishe huko au wazipeleke Baraza la Michezo (BMT), haiwezekani wachezaji hawapati morali kwa posho nzuri, hatutaelewana kwakweli'', ameongeza.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list