We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Monday, July 29, 2019

Kalemani apiga marufuku wananchi kulipia nguzo za umeme

Waziri wa Nishati Dk. Medard Kalemani, amesema wananchi hawapaswi kulipia nguzo wanapotaka kuunganishiwa umeme kwani hilo ni jukumu la Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco).
Akizungumza na wananchi katika Wilaya za Babati na Mbulu mkoani Manyara jana Julai 28, Waziri Kalemani pia ametoa onyo kwa mtumishi yeyote wa Tanesco atakayebainika kutomuunganishia umeme mteja aliyelipia huduma hiyo kwa kisingizio cha kutokuwepo nguzo au kumtaka alipie.
“Wananchi nchi nzima muelewe, hampaswi kulipia nguzo na kwamba atakayebainika kwenda kinyume na maagizo hayo ya serikali, atachukuliwa hatua za kinidhamu mara moja,” amesema.
Katika hatua nyingine Dk. Kalemani alitoa wito kwa wananchi vijijini, katika maeneo ambayo tayari miundombinu ya umeme imefika, kulipia Sh 27,000 tu ili waunganishiwe huduma hiyo.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list