We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Monday, July 8, 2019

IGP Sirro aagiza uchunguzi ajali iliyoua wafanyakazi watano wa Azam TV



Inspekta Jenerali wa Polisi nchini Tanzania (IGP), Simon Sirro ameagiza kufanyika uchunguzi kubaini chanzo cha ajali ya magari mawili iliyotekea eneo la Shelui mkoani Singida na kusababisha vifo vya watu saba wakiwemo wafanyakazi watano wa kampuni ya Azam Media.

Akizungumza jijini Mwanza leo Jumatatu Julai 8, 2019 katika ziara yake ya kukagua mradi wa ujenzi wa nyumba za polisi eneo la Myamhongolo, IGP Sirro ameuagiza uongozi wa jeshi hilo mkoani Singida kuchukua hatua za kisheria dhidi ya yeyote atakayebainika kuwa chanzo cha ajali hiyo iliyojeruhi wafanyakazi wengine wa kampuni hiyo.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa uzalishaji vipindi wa kampuni ya Azam Media, Yahya Mohamed, waliofariki dunia katika ajali hiyo iliyotokea asubuhi ya leo ni Salim Mhando, Florence Ndibalema, Said Haji, Sylvanus Kasongo na Charles Wandwi.
Madereva wa Coaster lililokuwa limewapakia wafanyakazi 10 wa kampuni hiyo, pamoja na dereva wa lori pia wamefariki katika ajali hiyo iliyotokea wakati wafanyakazi hao wakiwa njiani kwenda wilaya ya Chato Mkoa wa Geita nchini Tanzania kuripoti tukio la uzinduzi wa Hifadhi ya Taifa ya Chato-Burigi.
Uzinduzi wa Hifadhi hiyo unatarajiwa kufanywa kesho Jumanne Julai 9, 2019 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk John Magufuli.
Awali akizungumza askari katika uwanja wa Polisi Mabatini jijini Mwanza, IGP Sirro alikemea tuhuma ya vitendo vya rushwa na ukosefu wa maadili miongoni mwa baadhi ya askari huku akionya kuwa atachukua hatua za kinidhamu na kisheria dhidi ya askari yeyote wa ambaye ushahidi dhidi yake utapatikana.
Kuhusu wimbi la wahamiaji haramu katika baadhi ya visiwa ndani ya Ziwa Victoria, Mkuu huyo wa jeshi la polisi aliwaagiza Makamanda wa Polisi katika mikao ya kanda hiyo kuendesha operesheni maalum kuwakamata na kudhibiti wahamiaji haramu.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list