We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Monday, July 8, 2019

Chama cha Upinzani chashinda uchaguzi Ugiriki


Kiongozi wa upinzani wa chama cha kihafidhina nchini Ugiriki Kyriakos Mitsotakis ameshinda uchaguzi wa bunge uliofanyika jana Jumapili ambao umetoa pigo kwa waziri mkuu Alexis Tsipras aliyeiongoza Ugiriki kwa miaka minne wakati wa mzozo mkubwa wa kifedha.

Chama cha New Democracy cha mwanasiasa Mitsotakis kimepata asilimia 39.8 ya kura ikilinganishwa na asilimia 31.5 za chama cha mrengo wa shoto cha Syriza cha waziri mkuu Tsipras. Mitsotakis ambaye atakuwa waziri mkuu ajaye, ameahidi kupunguza kiwango cha kodi, kuvutia uwekezaji na kubuni nafasi zaidi za kazi.

 Kwenye uchaguzi huo, chama cha mrengo mkali wa kulia cha Golden Dawn ambacho kiliundwa na wanazi mamboleo kimeshindwa kurejea bungeni katika matokeo yanayoashiria kupotea uungwaji mkono wa chama hicho kilichokuwa cha tatu kwa ukubwa katika bunge la Ugiriki. 

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list