We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Thursday, June 27, 2019

Lema alitaka Bunge kumchukulia hatua Lusinde kwa kauli hii


Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema amesema anatarajia Bunge au Serikali kuchukua hatua kwa kauli aliyoitoa Mbunge Lusinde juu ya Wakenya kupigwa kama kujibu mapigo ya kauli la Jaguar.

Lema amesema yeye amefukuzwa Bungeni kwa vikao vyote mpaka 2020 kwa kuunga mkono kauli ya CAG na Halima Mdee juu ya udhaifu wa Bunge.

"Nimefukuzwa Bungeni kwa vikao vyote mpaka mwaka 2020,kwa kuunga mkono kauli ya CAG/Mh Mdee juu ya udhaifu wa Bunge, natarajia Bunge/Serikali kuchukua hatua kwa kauli aliyoitoa Mb L.Lusinde, juu ya Wakenya kupigwa kama kujibu mapigo kauli ya Mb Jaguar.Hili ni jaribu baya kwa EAC," ameandika Lema kwenye mitandao yake ya Kijamii.

Lema na Halima Mdee walisimamishwa kutohudhuria vikao vya Bunge kwa kuunga mkono kauli ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list