We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Thursday, June 27, 2019

Djuma asifu usajili wa Bigirimana Yanga

Aliyekuwa kocha wa AS Kigali Masudi Djuma amesema Yanga imepata mchezaji hasa baada ya kumsajili kiungo mshambuliaji Issa Bigirimana kutoka APR ya Rwanda
Djuma aliyewahi kufanya kazi Tanzania na klabu ya Simba, amesema anamfahamu Bigirimana vizuri na anaamini atapata mafanikio makubwa katika klabu ya Yanga
Djuma amesema kuwa anatambua uwezo wa mchezaji huyo, akiwa ameibuka mfungaji bora zaidi ya mara nne timu ya APR, hivyo anaamini atafanya mambo mazuri pia kwa Wanajangwani hao.
"Nimekuwa na Bigirimana katika timu zaidi ya tatu na nimekutana naye tena hapa APR, Rwanda, natambua uwezo wake ni mzuri, pia ni mchezaji ambaye anajiamini sana anapokuwa uwanjani," Djuma amenukuliwa na gazeti la Bingwa
"Hata hivyo, niliposikia anakuja Tanzania kujiunga na klabu ya Yanga, niliona wamepata kiungo mzuri ambaye atawasaidia kwenye plani zao"
"Bigirimana ni kama mdogo wangu, baada ya kufahamu anakuja Tanzania nimezungumza naye mambo mengi, lakini nimemsisitiza zaidi kufanya kazi nzuri ili azidi kijitengenezea njia ya kufika mbali"
Katika klabu ya Yanga, Bigirimana atakuwa na kiungo mwingine mshambuliaji Patrick Sibomana wakiwa wote wametokea Rwanda

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list