We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Thursday, May 2, 2019

Wawa aanza mazoezi, kurejea kikosini karibuni


Beki kisiki wa Simba Paschal Serge Wawa ameanza mazoezi mepesi tayari kurejea dimbani baada ya kuwa nje kwa zaidi ya wiki tatu


Wawa aliumia kwenye mchezo wa kwanza wa robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika kati ya Simba dhidi ya TP Mazembe uliopigwa uwanja wa Taifa
Wawa ameanza mazoezi binafsi na huenda akajumuishwa kwenye kikosi cha Simba kitakaporudi kutoka mkoani Mbeya

Mwenyewe amethibitisha kuwa hali yake inaendelea vizuri na tayari ameshaanza mazoezi binafsi

"Ninaendelea vizuri kwa sasa tofauti na awali na nimeanza mazoezi binafsi na sasa hivi ninafanya mazoezi ya Gmy," amesema
Simba imecheza michezo sita ya ligi bila ya Wawa na imefanikiwa kushinda michezo mitano

Walinzi Juuko Murshidi, Paul Bukaba na Yusufu Mlipili wameweza kutimiza ipasavyo majukumu ya ulinzi wa kati wakishirikiana na mkongwe kiraka Erasto Nyoni

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list