We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Thursday, May 30, 2019

Bulaya amhoji Waziri kutobomoa nyumba ya kigogo

Mbunge wa Bunda Esther Bulaya amehoji juu ya kutobomolewa kwa nyumba ya kigogo mmoja wa Kinondoni jijini Dar es salaam bila kutaja jina la mtu huyo kwa kile allichokidai zoezi hilo lilipaswa kutekelezwa muda mrefu lakini halijafanyika.

Esther Bulaya ametoa kauli hiyo Bungeni jijini Dodoma alipokuwa akiuliza swali kwa Waziri wa Ardhi William Lukuvi, kuhusiana na wananchi wanaojenga kwenye ya mikondo ya maji.
"Serikali imebomoa nyumba zilizojengwa kwenye mikondo ya mito, umebomoa nyumba nyingi Kawe, kuna nyumba ya kigogo imeachwa, lini itavunjwa?", ameuliza Bulaya.
Akijibu swali hilo Waziri Lukuvi amesema suala la ubomoaji wa nyumba Wizara inapokea orodha kutoka kwa Afisa Ujenzi wa Wilaya wao ni watekelezaji tu.
"Oda ya kubomoa inatolewa na Afisa Ujenzi Wilaya, mazoezi haya yamefanyika wilayani Kinondoni, bonde la Msimbazi naomba wananchi wasijenge bila vibali", amejibu Waziri Lukuvi.
Kwa sasa Bunge linaendelea jijini Dodoma ambapo Mawaziri mbalimbali wameendelea kuwasilisha makadirio ya bajeti kwa Wizara zao kwa mwaka wa fedha 2018/2019.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list