We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Saturday, March 23, 2019

YANGA: TUNABEBA UBINGWA MIKONONI MWA SIMBA NA KUSEPA NAO

BEKI wa timu ya Yanga, Abadlah Shaibu 'Ninja' amesema licha ya kikosi chake kupoteza mbele ya Lipuli mchezo wa ligi bado wana nafasi ya kubeba ubingwa ulio mikononi mwa Simba kwa sasa.

Ninja amesema kuwa kupoteza mchezo kwenye ligi haina maana ya kupoteza kasi ya kuendelea kupambana bali ni matokeo ambayo yanaikuta timu yoyote inayotafuta ushindi.

"Bado naiona timu yangu ikibeba ubingwa wa ligi msimu huu hivyo kupoteza kwetu mbele ya Lipuli hakujatuyumbisha bali kumetupa hasira ya kupambana kuyatafuta mafanikio.

"Bado tuna michezo mikononi na bado tunaongoza ligi sioni kitakachotufanya tupoteze kwa sasa hivyo mashabiki waendelee kutupa sapoti, wachezaji bado tuna nguvu na matumaini ya kufanya makubwa," amesema Ninja.

Yanga wamecheza michezo 28 wamepoteza michezo mitatu pekee na wametoa sare michezo minne  kwenye ligi huku wakiwa ni vinara wa ligi baada ya kukusanya pointi 67 kibindoni.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list