We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Sunday, September 15, 2019

Waiba choo cha Dhahabu

Choo cha Dhahabu kilichoundwa kwa Karati 18 chenye thamani ya zaidi Shilingi Bilioni 11.5 kimeibiwa, katika jumba la Bleinheim huko nchini Uingereza usiku wa kuamkia leo.


Choo hicho kilikuwa kikitumika kwa ajili ya maonesho na kumilikiwa na msanii Maurizio Cattelan, ambaye ni raia wa Italia, ambapo watu mbalimbali walikuwa wakitembelea na kulipia pesa ili ya kukitumia.
Kuibiwa kwa choo inaelezwa kuwa iligundulika hasa baada ya maji kuanza kutapakaa ndani ya jumba hilo, kutokana na kuondolewa kwa nguvu katika eneo ambapo kilikuwa kimewekwa na kuunganishwa na mifumo ya maji, kama choo cha kawaida kinavyokuwa.
Mpaka sasa mtu mmoja anashikiliwa na Polisi kwa mahojiano, huku jumba hilo likifungwa kwa muda kwa ajili ya uchunguzi zaidi na Polisi.
Chanzo: BBC

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list