Tunisia inatarajiwa kufanya uchaguzi wa rais leo. Hii itakuwa mara ya pili kwa nchi hiyo kufanya uchaguzi huru wa rais kwa njia ya demokrasia tangu kutokea vuguvugu lililotokea mwaka 2011 na kumuondoa madarakani aliyekuwa rais wa nchi hiyo, Zine el-Abidine Ben Ali.
Wagombea 26 akiwemo Waziri Mkuu Youssef Chahed watashiriki uchaguzi huo. Hata hivyo haijajulikana wazi ni nani atafaulu kuingia kwenye duru ya pili ya uchaguzi huo.
Wapiga kura milioni saba wanatarajiwa kushiriki uchaguzi huo, baada ya kumalizika rasmi kampeni zilozojikita zaidi kwenye changamoto za kijamii na kiuchumi zinazoizonga nchi hiyo ya Afrika kaskazini.
We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.
Subscribe to our RSS feed to stay updated on our progress.

No comments:
Post a Comment