Afisa Habari wa klabu ya Simba Haji Manara ameeleza kusikitishwa na kitendo cha mashabiki wa timu hiyo kupigwa na wenzao wa Yanga jana walipoenda kushuhudia mchezo wa ligi ya mabingwa kati ya Yanga dhidi ya ZESCO United
Manara amesema huo ni utamaduni wa hovyo ambao unafaa kukomeshwa kwani mashabiki hao walitumia utashi wao kwenda kushuhudia mchezo huo wakiwa wamevaa jezi za timu yao pendwa, Simba
"Shida ya Washabiki wa 'Kwala' hujiona wao wana haki zaidi ya wenzao"
"Wao walikuja kutuzomea mechi na UD Songo,walifanya hvyo na Nkana,Mbambane,Vita na hata Mazembe,hakupigwa mtu wao wala hakufanyiwa fujo"
"Kwa nini wafanye hivi,? alihoji Manara"
"Naamini mamlaka zitachukua hatua,wakiacha huu ujinga kuna siku tutalia na tusiowajua!! Poleni Wanasimba na Mungu kawajaalia kupenda klabu ya Watu waliostaarabika"

No comments:
Post a Comment