We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Tuesday, September 3, 2019

Mgambo waonywa kupiga wananchi

MKUU wa Wilaya ya Kilolo, Asia Abdallah, amepiga marufuku mgambo kutumia nguvu kupiga hadi kuumiza watuhumiwa wa makosa mbalimbali wanapowakamata.
Badala yake, amewataka kutumia akili zaidi badala ya mabavu yasiyohitajika katika ukamataji watuhumiwa.
Alisema mgambo kupewa jukumu la ulinzi na usalama wa wananchi, si kibali cha kuwanyanyasa au kuwapiga virungu na kuwajeruhi wakati wa kuwakamata.
Akizungumza katika Kijiji cha Ilawa jana, wakati wa kufungua mafunzo ya mgambo wa Kata ya Image, Asia alisema umezuka mtindo wa mgambo kugeuka miungu watu na kunyanyasa wananchi.
“Mimi tangu niwe mkuu wa wilaya hii, nina vyombo mbalimbali vya ulinzi, sijawahi kuagiza kupiga wananchi, nataka ninyi tumieni medani ya mafunzo mliyopewa katika kukamata watuhumiwa,” alisema.
Asia alisema siku zote nguvu hutumika pale mtuhumiwa anapotumia nguvu zaidi ambayo inaweza kuhatarisha usalama.
Alisema hatasita kuchukua hatua kwa mgambo yeyote atakayebainika ama kulalamikiwa na wananchi.
“Nikikukuta umetumia vibaya nafasi yako kwa kumpiga mwananchi au umetumia nguvu eneo ambalo nguvu haikuhitajika, nitakushughulikia,” alisema Asia.
Katika hatua nyingine, aliwaagiza mgambo kuendelea kuwa walinzi wa usalama katika vijiji vyao na kuchukua hatua ya kudhibiti majanga ya moto pindi yanapojitokeza.
Alisema kupitia mafunzo hayo, vijana wanaweza kujiajiri kwa kuanzisha vikundi vya ulinzi na vya kiuchumi.
Katika mafunzo hayo vijana zaidi ya 150 walihitimu

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list