Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems amesema mshambuliaji hatari wa timu hiyo Meddie Kagere alipata majeraha madogo kwenye mchezo dhidi ya Mtibwa Sugar
Kagere hakuwa sehemu ya wachezaji waliofanya mazoezi jana kwenye uwanja wa Gymkhana na kuibua maswali kuhusu alipo kinara huyo wa mabao
Hata hivyo Aussems amesema mchezaji huyo yuko chini ya uangalizi maalum kufuatia majeraha hayo
Aussems ameongeza kuwa kwa sasa safu yake ya ushambuliaji inamtegemea zaidi yeye kutokana na washambuliaji wengine John Bocco na Wilker Da Silva kutokuwa fiti
Hivyo wanalazimika kuwa makini na afya yake
Kagere ameanza msimu mpya kwa kishindo akiwa akiwa tayari amefunga mabao matatu katika michezo miwili aliyocheza

No comments:
Post a Comment