Beki Juma Abdul ambaye wiki iliyopita alifiwa na mama yake, amerejea kikosini kuendelea na maandalizi ya mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya ZESCO United
Abdul ameshiriki mazoezi ya jioni ya kikosi cha Yanga yaliyofanyika uwanja wa Nyamagana
Yanga imefanya mazoezi ya mwisho jijini Mwanza kabla ya kuanza safari ya kurejea jijini Dar es salaam
Nyota wengine waliorejea kikosini ni pamoja na Kelvin Yondani na Mohammed Issa 'Banka' waliokuwa na majukumu ya timu ya Taifa
Winga Patrick Sibomana na Farouk Shikalo huenda wakaungana na timu jijini Dar es salaam

No comments:
Post a Comment