We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Friday, August 16, 2019

'Wakulima wanahangaika sana' - RC Rukwa

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Joachim Wangabo amevitaka vyama vya ushirika katika Mkoa wa Rukwa kujiunga na Chama Kikuu cha Ushirika cha Mkoa, ili kuwa na umoja na nguvu katika kutafuta masoko ya mazao yao na kuachana na walanguzi.

Ameyasema hayo katika mkutano wa Vyama vya Ushirika mkoani humo, aliouitisha ili kuwatafutia wanachama wapya chama kikuu cha Ushirika cha Mkoa pamoja na kusikia mipango yao waliyojiwekea kuanzia mpango wa mwaka mmoja hadi miaka kumi.
Amesema kuwa Chama Kikuu cha Ushirika cha Mkoa 'Ufipa Cooperative Union Ltd (UCU)' ni chama kipya na kinahitaji nguvu ya vyama vya ushirika vya mkoa mzima ili kiwe na uongozi uliokamilika.
"Mkulima ana mahangaiko makubwa sana, sasa huu ushirika ni chombo cha kumkomboa mkulima, ni chombo cha kunyanyua uchumi wa mkulima, ni chombo cha kuikomboa Rukwa, ni chombo cha kuikomboa nchi yetu ya Tanzania, nchi ambayo sasa inaelekea kwenye uchumi wa kati wa viwanda", amesema Wangabo.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list