Waziri huyo wa Serikali ya Awamu hii ya Tano, amesema kwa mziki uliopo Jangwani kwa sasa, ubingwa lazima urejee Yanga baada ya misimu miwili watani wao Simba kulibeba wakiwapora msimu wa 2017-2018.
Mkuchika amekiri safari hii Yanga wana timu tishio na inapiga soka la kitabuni hivyo haoni kama kuna timu itagusa moto wao.
Mwenyekiti huyo alikuwepo uwanjani jana huku akiridhika na matokeo ya sare ya bao 1-1 iliyopata timu yake dhidi ya Kariobangi Sharks ya Kenya.
Amesema licha ya kwamba matokeo yalikuwa sare lakini ameridhika na kiwango kikubwa kilichoonyeshwa na wachezaji wa Yanga huku wakimiliki mpira kwa vipindi vyote viwili.
"Tulimiliki mpira sehemu kubwa ya mchezo,wachezaji wamecheza vizuri sana ndio maana unaona licha ya sare lakini mashabiki wameridhika na soka waliloliona.
Alisema wanajivunia mwaka huu timu wanayo na wapinzani watapata tabu sana na wale waliochukua ubingwa msimu uliopita wanatakiwa kuwapisha kwani wenye nafasi yao wanarudi msimu huu.
"Tunashiriki ligi kwa sababbu tunataka ubingwa na tumezoea kuwa mabingwa kwani hata ukiangalia wapinzani wetu wakubwa ambao tunashindana nao kwenye mbio za ubingwa hawatufikii kwa kuwa sisi tumechukua Kombe mara nyingi"alisema Mkuchika.

No comments:
Post a Comment