We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Monday, August 5, 2019

Okwi awaaga mashabiki wa Simba, atoa ahadi

Mshambuliaji wa zamani wa Simba Emmanuel Okwi ambaye ni raia wa Uganda, ameiaga rasmi klabu ya soka ya Simba akiwa tayari kwenda kuanza maisha mapya ndani ya klabu ya Itthad Alex SC ya Misri na kuahidi timu hiyo itabaki moyoni mwake.

Kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii, Okwi ameweka ujumbe wa kuwashukuru mashabiki kwa kumpenda na kumfanya ajisikie nyumbani kwa miaka yote ambayo amechezea klabu hiyo.
''Niwashukuru mashabiki kwa kila kitu ambacho mmenifanyia, mmekuwa watu wazuri sana kwangu, nawahakikishia kuwa upendo wenu kwangu nautambua'', ameandika Okwi.
Okwi ambaye ameichezea Simba tangu mwaka 2010, amelishukuru pia benchi la ufundi pamoja na viongozi wa Simba kwa ushirikiano ambao wamekuwa wakiwapa ili kufikia malengo yao binafsi na ya klabu.
''Ninawaahidi kuwa nakwenda Itthad Alex SC lakini Simba itabaki moyoni mwangu'', ameongeza.
Okwi ameichezea Simba kwa misimu isiyopungua 6 na kufunga magoli zaidi ya 70, huku akichukua makombe kadhaa ikiwemo Ligi kuu, Kombe la shirikisho nchini na mengine.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list