We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Thursday, August 1, 2019

Mazoezi kikosi cha Zimamoto yazua taharuki Bukoba


Taharuki ilitanda leo Alhamisi  Agosti Mosi, 2019 wakati Jeshi la Polisi Kikosi cha Zimamoto na Uokoaji kikifanya mazoezi ya kuzima moto katika uwanja wa ndege wa Bukoba.

Hali hiyo iliwafanya wananchi kuamini kuna ndege imeanguka, kuchochewa zaidi na magari ya kikosi hicho  yaliyokuwa yakielekea na kutoka katika uwanja huo, yakiwa yamepakia watu waliokuwa wakiigiza kama majeruhi waliokuwa wakipelekwa hospitali.
Evarista Mutasingwa wamesema aliamini ni tukio la kweli baada ya ulinzi mkali kuimarishwa na magari ya usalama kuongezeka.
Zoezi hilo lililoshirikisha vikosi mbalimbali halikujulikana na limetajwa kama hatua ya kupima utayari iwapo litatokea tatizo linalohitaji kukabiliwa kwa mazingira ya dharura.
Akizungumza na Mwananchi kamanda wa kikosi hicho mkoani Kagera, Hamis Dawa  amesema wamefika mapema kwenye eneo la tukio na kushiriki kuzima moto na shughuli za uokoaji.


Ametaja baadhi ya changamoto zilizobainika kuwa ni uchache wa magari ya kusafirisha wagonjwa na  wataalamu wa afya katika hospitali walikopelekwa  majeruhi wa ajali hiyo.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list