We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Friday, July 12, 2019

Wana - CCM watakiwa kumuunga mkono Rais Magufuli


Na Timothy Itembe, Mara

Mbunge wa viti maalumu Tanzania kupitia Chama cha mapinduzi CCM,Amina Makilagi amewataka wanachama wa Chama cha mapinduzi CCM kumuunga mkono Rais awamu ya Tano,DT John Pombe Magufuli katika juhudi za kutekeleza shuguli za maendeleo kwa jamii.

"Shuguli za maendeleo kwa jamii anazotekeleza Rais John Pombe Magufuli wanachama wa Chama cha Mapinduzi kuna haja ya kumuunga mkono kwasababu lengo ni Taifa letu kuondokana na umasikini,Ujinga huku tukipambana na  maradhi na kwa kuwa mimi ni Mbunge ambaye ninatokana na CCM Mmi ni wa  kwanza kumuunga mkono Rais wetu kulingana na katiba yetu"alisema Makilagi.

Makilagi aliongezsa kuwa Rais Magufuli na viongozi wengine waliotangulia kabla yake wamefanya kazi kubwa ya kujenga Taifa la Tanzania ili kuhakikisha kwamba Wananchi wake wanapata hudumas mhimu za kijamii huku wakinufaika na matunda ya Uhuru wao.

Pia Mbunge huyo aliongeza kuwa Rais Magufuli ametekeleza miradi mikubwa ndani ya Tanzania na amejenga imani kwa Watanzania pamoja na Mataifa mengine anasifika kuwa kiongozi Bora.

Makilagi alitumia nafasi hiyo kuchangia Ofisi ya Jumuia ya Wanawake Tanzania UWT Wilaya Tarime  Kumpyuta  mashine ikiwa na vifaa vyake  kwa lengo la  kuchapisha machapisho pamoja na kuandalia  taarifa mbalimbali za kiofisi Ofisini kwao na kuondokana na kero ya kwenda kuandaa taarifa za Jumuia ya UWT  kwenye vibanda vya watu binafsi ambavyo sio sehemu salama.


Kwa upande wake Katibu wa Chama cha mapinduzi wilayani Tarime mkoani Mara,Khamisi Mkaruka alisema kuwa licha ya kuwa wilaya Tarime kwa maana ya majimbo yake mawili Tarime Vijijin inayoongozwa na John Heche na Tarime Mjini iliyo chini ya Esther Matiko chini ya Upinzani kwa maana ya Chama cha Demokrasia na maendeleo Chadema wanaimani kuwa majimbo hayo kwa uchaguzi ujao yanaenda kurudi ndani ya CCM.

Mkaruka aliongeza kuwa kwenye uchaguzi wa Serikali za mitaa Chama chake kimejipanga kuhakikisha kuwa Chama hicho kinaenda kupata viti vingi tofauti na uchaguzi wa mwaka uliopita ambapo upinzani kwa maana ya Chadema walikuwa na viti vingi hata kuongoza halmashauri kwa maana ya madiwani wake kuwa wengi. 

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list