We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Wednesday, July 3, 2019

Wabunifu kufuatwa vijijini

Serikali imeagiza wabunifu mbalimbali nchini kufuatwa maeneo ya vijijini ili waweze kuonesha kazi zao kutumika na kuleta manufaa kwa taifa.
Hayo yameelezwa leo Jumatano Julai 2, na Naibu Waziri wa Wizara ya Elimu, Sayansi Teknolojia na Ufundi, William Ole Nasha alipokuwa katika banda la maonesho la Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) ambapo amewataka  kuongeza nguvu ya kuwafuata wabunifu waliopo maeneo ya vijijini na kuwasaidia kuonekana kwa kazi zao.
“Nimetembelea mabanda takribani nane yaliyokuwa chini ya wizara hii lakini nimeona kuna wabunifu wengi wapo na wanabuni kazi mbalimbali zenye uwezo mkubwa wa kusaidia taifa hili hivyo ni vyema wakafuatwa katika maeneo yao na Costech mkawa katika mstari wa mbele kuwasaidia wabunifu hao.
“Mfano nikiwa katika banda la Mamlaka ya Elimu na Ufundi Stadi (VETA) nimeona wabunifu wa mitambo ya umeme unaosaidia katika masuala mbalimbali ya kiusalama hii itasaidia mkaweza hata kuwapa mitaji wakafanya vizuri zaidi kwa kushirikiana na mashirika makubwa kama Shirika la Umeme nchini (Tanesco),” amesema.
Katika banda la VETA kuna mbunifu amefanikiwa kutengeneza mfumo unaopiga simu wenye kama eneo la nyumba lina hatari ikiwamo gari au lifti.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list