We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Wednesday, July 10, 2019

Tanzania yatangaza awamu ya tatu uhakiki taasisi za kidini, jumuiya za kijamii



Wizara ya Mambo ya Ndani nchini Tanzania itaanza awamu ya tatu ya uhakiki wa taasisi za kidini na Jumuiya za Kijamii katika mikoa mitano kuanzia Julai 15 hadi Julai 24 mwaka 2019.

Usajili huo utafanyika katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya huku ukihusisha mikoa ya Mbeya, Iringa, Njombe, Rukwa na Songwe.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana Jumanne Julai 9, 2019 na Katibu Mkuu wa Wizara ya mambo ya ndani ya nchi, Meja Jenerali Jacob Kingu ieleza shughuli hiyo itakuwa ikifanyika kuanzia saa mbili kamili asubuhi hadi saa 10 jioni.
“Taasisi itatakiwa kuwasilisha cheti halisi na kivuli chake, stakabadhi ya malipo ya ada ya hivi karibuni, katiba ya jumuiya/taasisi husika iliyopitishwa na msajili, barua inayothibitisha uwepo wa jumuiya hiyo kutoka kwa ofisa mtendaji wa Mtaa/kijiji ofisi ilipo,” alisema Kingu
“Taasisi ambazo zitashindwa kuhakikiwa kwa mujibu wa ratiba ya eneo zitalazimika kwenda makao makuu ya wizara Dodoma kwa uhakiki na iwapo zitashindwa kufanyiwa uhakiki kwa muda uliopangwa zitaondolewa katika orodha ya msajili.”


Awamu ya kwanza ya usajili wa taasisi hizo ulifanyika katika mikoa ya Dar es Salaama na Pwani huku awamu ya pili ikihusisha mikoa wa Morogoro,  Dodoma, Singida na Manyara.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list