We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Wednesday, July 10, 2019

Tanzania kufundisha Kichina shuleni na vyuoni

Baada ya mahusiano mazuri ya kiuchumi kati Tanzania na China,  serikali kupitia  wizara ya elimu  sayansi na Teknolojia imeona umuhimu wa matumizi ya  lugha ya kichina hapa nchini.


Hilo limebainishwa na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Avemalia Semakafu, amabapo ameeleza kuwa serikali imeamua kuifundisha lugha hiyo shuleni na vyuoni, ambapo kwa mwaka huu shule 16 zinatarajia kufanya mtihani wa taifa wa  lugha ya Kichina.
Akiongea katika uzinduzi wa kituo cha mafunzo ya Kichina  chuo kikuu cha Kiisilamu Morogoro (MUM), Semakafu amesema, ''Tanzania kufundisha lugha ya kichina ni muendelezo wa kuimarisha mahusiano yaliyokuwepo hapo awali toka kipindi cha Hayati Mwalimu Julius Nyerere na kituo hiki kitakuwa  cha tatu kati ya vituo vitakavyokuwa vinafundisha lugha hii ikiwemo chuo kikuu cha Dodoma na chuo kikuu cha Dar es salaam''.
Kwa upande wake Mwalimu idara ya elimu ya sanyansi nchini China He yozhou, amesema mbali na Tanzania na China kushirikiana kiuchumi wameongeza ushirikiano kwenye lugha, ambapo mpaka sasa China imetoa walimu zaidi ya 130 ili waje Tanzania kufundisha lugha ya kichina.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list