We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Sunday, July 28, 2019

Spika Mstaafu Anne Makinda Atoa Ushauri kwa Madiwani Wanawake

Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Anne Makinda, amewataka wabunge na Mdiwani wa vitimaalum nchini kusimamia kikamilifu rasilimali za umma ili ziwanufaishe wananchi wote.

Akizungumza Jijini Mwanza katika semina ya kujenga uwezo kwa viongozi wanawake wa serikali za Mitaa (WASEMI) iliyoandaliwa na shirika la TGNP Mtandao, Makinda alisema kwamba, mchango wa wabunge na madiwani wa viti maalum umekuwa hauonekani vizuri au kutambuliwa na jamii kutokana na wao wenyewe kuwa na hofu au kutokujiamini kitu ambacho kimechangia kuwarudisha nyuma na kushindwa kuendelea mbele.

“Tatizo letu sisi viongozi Wanawake, tunajenga hofu, tunaogopa sana kujitokeza na kuwajibika vizuri kwa wananchi, eti kwa sababu ni viti maalum. Sisi tulianzia pia viti maalum , lakini tulipata nafasi ya kwenda jimboni kwasababu tulijiamini, tuliwajibika kikamilifu na tulihangakikisha uwezo wetu unaonekana na kila mmoja. Jitokeze, kwa wananchi, watumikie kwa uadilifu na watakuona na kutambua mchango wako” alisema Makinda

Makinda amewaasa wanawake viongozi wa serikali za Mitaa, kuhakikisha wanasimamia ubora wa huduma za jamii kwenye halmashauri zao na kuhakikisha kila kinachofanyika kwenye halmashauri wanakielewa vizuri na kutoa taarifa kwa wananchi wote.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list