We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Saturday, July 27, 2019

RC kuwaweka kitimoto DC Sabaya na wafanyabiashara

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Mghwira, amesema amekutana na Mkuu wa Wilaya ya Hai Lengai Ole Sabaya na kumsikiliza dhidi ya shutma zilizotolewa na mfanyabiashara kuwa amemuomba rushwa ya shilingi milioni 5, ambapo Mghwira amewataka viongozi wabadilike.

Mghwira amesema kumekuwepo na malalamiko mbalimbali ya wafanyabiashara dhidi ya watendaji tofauti tofauti wa serikali, kutoka katika idara mbalimbalimbali hali inayoashiria ukwamishaji wa masuala ya biashara kwa nchi.
''Nimemsikiliza DC yeye kama yeye sasa itabidi tuwaite wote kwa vile wafanyabiashara wamelalamika hadharani na imebidi na sisi kamati ya usalama ya Mkoa tuwaite tuwasikilize ili watueleze kama kuna kero zingine tuzipunguze'' amesema Mghwira.
Julai 22 katika mkutano wa Kamishna wa Mamlaka ya Mapato (TRA) Mkoa wa Kilimanjaro na wafanyabiashara wa mkoa huo, mfanyabiashara huyo alidai kwamba DC Sabaya alimpa vitisho na kutaka ampe rushwa ya kiasi cha shilingi milioni 5. Baadaye Sabaya alizijibu shutma hizo kwa kusema si kweli.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list