We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Tuesday, July 9, 2019

Nawaambia zaeni tu, ndio maana uchumi wa China upo juu - Rais Magufuli


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amesema kadiri idadi ya Watanzania inavyoongezeka ndivyo na uchumi nao unakua.

Ameyasema hayo leo wakati akizindua Hifadhi ya Taifa ya Burigi-Chato iliyotokana na kuunganishwa kwa Mapori ya Akiba matatu ambayo ni Burigi, Biharamulo na Kimisi katika Mikoa ya Geita na Kagera.

"Nawaambia zaeni tu,ukishakuwa na idadi kubwa umetengeneza uchumi ndio maana uchumi wa China upo juu kutokana na population,najua nikizungumza hili wale watu ambao wamezoea kubania mayai watalalamika sana, nyinyi yaachieni waacheni wayabanie ya kwao" amesema Rais Magufuli.

Katika hatua nyingine Rais Magufuli amesema, “Idadi ya tembo imeongezeka kutoka 43330 mwaka 2016 hadi kufikia zaidi ya 60000 pia faru wameongezeka kufikia 163 hivyo hatuna budi kumpongeza Faru Rajabu (mtoto wa faru John) ambae ameshazalisha watoto 40 nadhani yule wajina wangu alikuwa hajitumi vizuri".

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list