We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Tuesday, July 9, 2019

Dk Tulia awatolea uvivu wanaoichukia Serikali ya Tanzania


Naibu Spika wa Bunge la Tanzania, Dk Tulia Ackson amesema wapo watu wana chuki na Serikali bila kujua, kisha chuki hiyo wanawaambukiza watoto wao.

Amesema hayo leo Jumanne Julai 9, 2019 kwenye kongamano la amani linalofanyikia kwenye Maonyesho ya 43 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (DITF) maarufu sabasaba jijini Dar es Salaam, Tanzania.
Dk Tulia amesema taifa bora ni lile linalolinda na kuthamini amani na kuthamini uhuru wa wengine pasi na kuwaumiza wengine.
Amesema uhuru wa mtu unaishia kwenye pua yake na  ukizidi hapo unamuumiza mtu mwingine kwa kumfanya akose amani binafsi na kuiweka nchi kwenye taharuki.
"Tunataka nchi ikue zaidi kwenye taswira ya viwanda tusingependa watu wanaochochea machafuko" amesema.
Amefafanua miongoni mwa wananchi wapo wanaovunja amani na hawataki nchi iwe na amani.
"Tujiepushe na hayo ili tusitumbukie kama taifa kwenye vitendo vya uvunjifu wa amani, tuna nafasi ya kuwafundisha watoto wetu umuhimu wa amani," amesema.
Dk Tulia amewaasa kwenye jukumu la kuhudumia wananchi wawahudumie kwa namna ambayo hawatakosa amani.
Ameeleza iwapo kuna huduma wanahitaji inayowezekana kupatikana leo ipatikane badala ya kuambiwa warudi kesho na kuwa na vinyongo mioyoni mwao.
"Usipomuhudumia ipasavyo akakosa amani, atawafanya na wengine kuikosa pia" amesema.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list