We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Sunday, July 28, 2019

Mbatia: Upinzani sio uadui

Mwenyekiti wa Chama cha NCCR Mageuzi nchini Tanzania, James Mabatia amesema upinzani si uadui bali ni fursa muhimu kwa viongozi kubadilishana fikra.
Mbunge huyo wa Vunjo ametoa kauli hiyo jana asubuhi Julai 27, 2019 katika mkutano mkuu wa  NCCR Mageuzi unaofanyika jijini Dar es Salaam.
“Mimi naona wewe unataka kuongoza hivi, mimi nina mawazo mbadala ya kuweza kuboresha hili kwa ajili ya maendeleo endelevu ya watanzania  ndiyo maana ya upinzani. Kunapokuwa na changamoto ya upinzani. Taifa linaneemeka zaidi.”
“Ndiyo maana leo kutoka sakafu ya moyo wangu huu upinzani tunasema si uadui, lazima tukubaliane. Mabadiliko yote yanaanza katika mabadiliko ya kifikra,” amesema Mbatia.
Katika hatua nyingine, Mbatia ametumia jukwaa hilo kuwaomba radhi Watanzania baada ya chama hicho kuwa kimya kwa muda mrefu bila kuonyesha mbwembwe zozote.


“Tulijitafakari na tafakari yetu hadi jana kuhusu mabadiliko katika fikra. Niwe mkweli mimi sijazaliwa kuwa mwenyekiti wa kudumu wa NCCR Mageuzi. Ningetamani kuona mwanamke ili kutekeleza kwa vitendo malengo ya kidunia,” amesema.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list