We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Friday, July 26, 2019

Mabingwa wa Burundi kucheza na Yanga Morogoro

Yanga inatarajiwa kucheza mchezo wa nne wa kirafiki kesho Jumamosi dhidi ya mabingwa wa Burundi, Aigle Noir.
Ikiwa kambini mkoani Morogoro, Yanga itacheza mechi hiyo ambayo itakuwa ni ya kwanza kukutana na timu kutoka nje ya nchi.
Mratibu wa Yanga, Hafidh Saleh amesema bado kocha wao msaidizi Noel Mwandila anahitaji mechi za kirafiki kukipima kikosi chake.
Saleh amesema mchezo huo utapigwa uwanja wa Highland Park ambao Yanga inautumia kwa mazoezi ambapo mabingwa hao tayari wametua Morogoro.
Aidha, Hafidh amesema pia kuna uwezekano mkubwa siku ya Jumapili Yanga itacheza na Mawenzi Market inayoshiriki ligi daraja la pili
Noir tangu watue nchini wamecheza mechi tatu za kirafiki dhidi ya Namungo FC, Kagera Sugar na Mtibwa Sugar walipoteza mbili na kutoa sare moja.
Timu hiyo awali ilifungwa na Namungo kisha kupokea tena kipigo kutoka Kagera zote wakifungwa mabao 3-0 kabla ya kutoa sare ya mabao 2-2 dhidi ya Mtibwa Sugar.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list