We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Wednesday, July 3, 2019

Hiki ndicho Lema atakachokisema akikutana na Rais Magufuli


Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema amesema siku akikutana wa Rais wa Tanzania, John Magufuli atamueleza jinsi viongozi aliowateua walivyojaa hofu na kushindwa kufanya uamuzi.

Lema akizungumza na wananchi wa jimbo lake amesema hofu hiyo inawafanya viongozi kushindwa kufanya uamuzi, kwamba hofu hiyo sasa imewakumba hadi wanasiasa ambao baadhi wanalazimika kuhama vyama vyao na kutokuwa wa kweli.

Amesema Chadema kinawataka viongozi walioteuliwa na kiongozi mkuu huyo wa nchi kuondoa hofu katika utendaji wao wa kazi ili waweze kutekeleza shughuli za maendeleo wanazozisimamia.

Akizungumza katika mkutano huo, Diwani wa Ngarenano (Chadema), Isaya Doita amesema  maendeleo katika jijini Arusha yanatokana na kazi nzuri ya baraza la madiwani la Chadema.

Lema alisimamishwa kuhudhuria mikutano mitatu ya Bunge kutokana na kuunga mkono kauli ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Mussa Assad kuwa Bunge la Tanzania ni dhaifu. 

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list