We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Sunday, July 7, 2019

DC Kusini Unguja ampa saa 48 mfanyabiashara kurejea Tanzania Bara



Mkuu wa Wilaya ya Kusini Unguja, Idrissa Kitwana Mustafa amempa saa 48 mfanyabiashara, Salome John kuondoka visiwani Zanzibar, kurejea Tanzania Bara.

Amedai mwanamke huyo aliwachukua wasichana kutoka Tanzania Bara kufanya kazi kwenye baa iliyopo Zanzibar, badala yake alikuwa akiwatumikisha kingono.
Akizungumza na Mwananchi leo Jumapili Julai 7, 2019 amesema amechukua uamuzi huo kwa kuwa kitendo kilichofanywa na mwanamke huyo ni kinyume na sheria za nchi, kubainisha kuwa kwa sasa mwanamke huyo anashikiliwa na kutoweka wazi mahali alipo.
Amebainisha kuwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) haipo tayari kuona wananchi wanateseka kwa ajili ya maslahi ya watu wachache, huku wakifanyishwa shughuli kinyume na matakwa yao.
Amesema mwanamke huyo alikuwa akiishi Kizimkazi Mkoa wa Kusini Unguja ameshahojiwa na Wizara ya Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Wanawake na Watoto.
“Kama kuna haki anazodaiwa na wasichana aliowachukua huko Tanzania Bara aweze kuwalipa kwa mujibu wa sheria za kazi,” amesema.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list