Watu 7 wamefariki dunia na watatu wamejeruhiwa, katika ajali iliyotokea eneo la Malendi Iramba mkoani Singida.

Picha ya ajali
Taarifa zinaeleza kuwa watu hao ni waandishi wa habari waliokuwa katika safari ya kikazi, wakielekea Chato mkoani Geita. Kwa mujibu wa Mganga Mfawidhi, Hospitali ya Wilaya ya Igunga, Tabora.
Naye Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Sweetbert Njewike amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo, ambapo gari dogo walilokuwa wamepanda wafanyakazi hao limegongana na lori lililokuwa likitoka Igunga kuelekea Dar es salaam.
Miongoni mwa vifo hivyo ni pamoja na wafanyakazi wa Azam Media, Salim Mhando, Florence Ndibalema, Said Haji, Sylvanus Kasongo na Charles Wandwi, wengine ni dereva na utingo wake ambao majina yao hayajafahamika.
Majeruhi ni Mohamed Mwinshehe, Mohamed Mainde ambao wapo ICU pamoja na Artus Masawe ambaye yake ni nzuri kiasi.
No comments:
Post a Comment