Ratiba ya Ligi inaonyesha Simba itacheza na JKT Tanzania Agosti 23 mchezo wake wa kwanza huku ratiba ya Shirikisho la Soka Afrika (CAF) ikionyesha timu hiyo itacheza mechi ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa dhidi ya UD Songo ugenini kati ya Agosti 23-25.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi, Boniface Wambura amesema, wakati wa kupanga ratiba ya Ligi Kuu hawakutarajia kama Simba ingeanzia hatua ya awali kwenye Ligi ya Mabingwa ndiyo sababu waliwapangia kucheza mechi za ufunguzi za Ligi Kuu.
"Kwa kuwa Simba ilitolewa katika robo fainali ya Ligi ya Mabingwa, tulitegemea wakianza mashinmdano ya CAF msimu ujao hawataanzia hatua za awali na imekuwa tofauti," alisema.
Alibainisha kwamba, kutokana na ratiba hiyo, watakaa na Simba na kuweka mambo sawa ili kuona ni namna gani watacheza mechi hiyo ya ufunguzi wa Ligi.
Awali, Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe alieleza namna alivyochukizwa na viporo vya Ligi ya msimu uliokwisha.
"Kwa namna viporo vilivyokuwa vingi, Ligi yetu ingeingia hata kwenye kitabu cha maajabu ya dunia, tumelijadiri hilo na TFF na Bodi ya Ligi ambao wamenihakikishia kuwa hilo halitojirudia," alisema Dk Mwakyembe.

No comments:
Post a Comment