We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Thursday, June 27, 2019

Wanaouza ramani za majengo mitaani wapigwa marufuku


Mwenyekiti wa Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi (AQRB) nchini Tanzania, Dk Ludigija Bulamile amesema ni kosa kisheria kwa watu kuuza ramani za majengo mitaani.

Dk Bulamile ameyasema hayo leo Alhamisi Juni 27, 2019 jijini Dar es Salaam wakati wa mafunzo kwa waandishi wa habari kuhusu majukumu ya bodi hiyo katika kusimamia ujenzi wa majengo bora na salama kwa umma.
Amesema ramani za majengo zinatengenezwa baada ya mtaalamu (mbunifu majengo) kufika kwenye ardhi husika ambako jengo hilo litajengwa ili kuona ardhi yake, kama kuna mkondo wa maji au upepo unavuma kuelekea upande gani.
"Kisheria ni kosa kuuza michoro ya majengo, kwa hiyo tunashauri watu wasinunue michoro mitaani bali wawaone wabunifu majengo. Hii ni kwa ajili ya usalama wa nyumba zao na ujenzi unaofuata mpangilio," amesema mwenyekiti huyo.
Dk Bulamile ameongeza ni kosa kisheria kujenga jengo bila kuwatumia wabunifu majengo na wakadiriaji majenzi.


Amesema katazo hilo la kisheria linawahusu wanaojenga nyumba zenye thamani ya zaidi ya Sh150 milioni au majengo yanayotumiwa na watu wengi kama vile shule, kanisa au msikiti.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list