We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Friday, June 21, 2019

Video: Tahadhari kama hizi zisipuuzwe, Marekani wanasiri kubwa- Chadema

Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimesema kuwa tahadhari iliyotolewa na ubalozi wa Marekani nchini isipuuzwe.
Hayo yamesemwa jijini Dar es salaam na Mkurugenzi wa Itikadi na Uenezi wa Mambo na Nje, John Mrema alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari, ambapo amesema kuwa taarifa kama hizo hazipaswi kupuuzwa.
Amesema kuwa Marekani imekuwa ikitoa taarifa mbalimbali katika balozi zake duniani kote ili kuweza kuwalinda raia wake.
”Lengo kubwa la Marekani ni kuwalinda raia wake, ukiangalia tukio la mashambulizi kama lililotokea London, Ufaransa, New Zealand hata hapo kwa majirani zetu Kenya, Wamarekani walitoa taarifa, na kweli mashambulio ya kigaidi yaliyotokea, ombi letu taarifa hizi zisipuuzwe,”amesema Mrema
Hata hivyo, Mrema ameongeza kuwa taarifa kama hizo za kiusalama, hazitakiwi kutolewa kwa kificho bali zinatakiwa kutolewa hadharani ili hatua stahiki zichukuliwe.



No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list